Boom Fresh | Hizi ndizo ngoma ambazo zimeachiwa na zinapatikana Boomplay wiki hii
Leo ni Ijumaa ya murua kabisa, siku ambayo huwa tunakusogezea ngoma ambazo zimeachia wiki nzima kwaajili ya kukukumbusha kusikiliza ngoma hizo endapo utakuwa umepitwa kutokana na shughuli mbalimbali za kila siku.
Wiki hii tumeshuhudia wasanii wakiachia ngoma mbalimbali. Wasanii hao ni Ommy Dimpoz (Dedication Album), Nay Wa Mitego (Sauti Ya Watu), Hemedy PHD (Carolina), Nuh Mziwanda (Penzi Jipya), Drimo (Bongo Pop Vol 1 EP).
Ommy Dimpoz - Dedication
Staa wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz ameachia albamu yake ya kwanza 'Dedication' baada ya kupita muda mrefu bila kuachia project kubwa yoyote. 'Dedication' ni albamu yenye ngoma 15 zenye mchanganyiko wa ladha za muziki mbalimbali. Ngoma zilizomo kwenye albamu hii ni 'Birthday', 'Mon Babe', 'Hasara Roho', 'I Got You', 'Magdalene', 'Moyo', 'Mpela Mpela', 'My Woman', 'Wale Wale', 'Marry You', 'My Queen', 'Ngolowane', 'Anaconda', 'Zekete' na 'Vacation'. Vile vile wasanii walioshirikishwa kwenye albamu hii ni Princess Nandy, Marioo, Musa Keys na DJ Maphorisa kutoka South Africa, Fally Ipupa kutoka DR Congo, na wengine wengi.
Nay Wa Mitego - Sauti Ya Watu
Rais Wa Kitaa, Nay Wa Mitego amerejea tena kwa mashabiki wake baada ya kuachia ngoma yake mpya 'Sauti Ya Watu'. Ngoma hii imekuja ikiwa imepita takribani miezi miwili tangu alipoachia albamu yake ya 'Rais Wa Kitaa'. 'Sauti Ya Watu' ni ngoma kali ambayo imejikita katika kuzungumzia changamoto mbalimbali wanazokabiliana wananchi hususani Watanzania.
Hemedy PHD - Carolina
Hemedy PHD amewakumbuka wafuasi wake baada ya kuja na ngoma mpya ambayo ameipa jina la 'Carolina' Remix akimshirikisha Ben Pol. Hii ni ngoma yake ya kwanza kwa mwaka huu wa 2022. Ni ngoma nzuri ambayo ni vizuri kuipitisha kwenye masikio yako.
Nuh Mziwanda - Penzi Jipya
'Penzi Jipya' ni ngoma mpya kutoka kwa Nuh Mziwanda. Ni ngoma yake ya tano kwa mwaka huu wa 2022. Sikiliza ngoma hii hapo chini kutoka Boomplay.
Penzi Jipya ft. Ucho & Muki Comando
Drimo - Bongo Pop Vol 1 EP
Msanii chipukizi anayekuja vizuri, Drimo amedondosha EP yake mpya inayojulikana kwa jina la Bongo Pop Vol 1. 'Bongo Pop Vol 1' ni EP yenye ngoma nne ambazo ni 'Romeo & Juliet', 'Wapi', 'Mi Lover' pamoja na 'Nilewe'.
#BuzzBrandColumn #BoomFresh #Music #Trending
Comments (40)
New Comments(40)
Angel Sangaxzzo5
dauddt1c8
rais!!!
Thomas kingwaluye1kp
nay wamitego sauti yawatu[0x1f627][0x1f608][0x1f621]
Ivan boyywn1p
napend san
Ramadhani Mlanziqu1a1
ngoma kali wako vizur big up all artist
149619931
[0x1f608][0x1f608][0x1f608][0x1f608]mamb[0x1f627][0x1f627]
Ashery Wilbard
bongo sie wanafiki tu yani full masifa hata kama mtu hajaweza mtampamba na kisha nae anabweteka kwamba anayaweza badala mmwambie ukweli dah! maie naomba nisiwe mnafika hakuna big up kwa nay tu wengine wakaze but
Mkw@bi offici@l
raisi wa kitaa big up brother
hamisicostantine@gmail.c
duhh! aisee wame tisha kinyama
Gif Ttyh9ffc
Cool
George Gilayo
sema huyu nay kaua kichizi kwa hili jiwe
iddywalocation
Ngoma Zote Nikali Wenyewe wapambane tunawapenda Natunawaombea Wafike Mbali Kimuziki
jamani mbona hauvumi hivi