Boom Top: Ngoma kali kumi zilizofanya vizuri zaidi Boomplay wiki iliyopita hizi hapa!
Leo ni Jumatatu murua, siku ambayo tunamulika ngoma ambazo zimefanya vizuri ndani ya orodha ya ngoma 100 wiki iliyopita.
Katika kuhakikisha hili linakwenda vizuri, tunakusogezea ngoma 10 ambazo zimeongoza kwenye chati wiki iliyopita.
1. Kwikwi - Zuchu
Ngoma hii kutoka kwa Zuchu Kwikwi ni ya Mapenzi ambayo Zuchu anaonesha ni kwa kiasi gani anampenda mpenzi wake huku akimsihi mpenzi wake huyo asimuache kwani anaogopa kuumbuka na kupata aibu mbele za watu.
2. Nakupenda - Jay Melody
Ni ngoma kali kutoka kwa Jay Melody huku ikiwa ni miongoni mwa ngoma zinazochezwa sana kwa sasa kwenye majukwaa mbalimbali ya muziki. Imeendelea kubaki nafasi ya pili kama ilivyokuwa wiki iliyopita.
3. Nitaubeba - Harmonize
Kwa mara ya kwanza ngoma hii iliingia kwenye kumi bora zaidi ya mwezi mmoja uliopita. Ngoma hii kutoka kwa Harmonize imeendelea kukubalika kwa mashabiki wengi Tanzania na nje ya Tanzania.
4. Zuchu - Love ft Adekunle Gold
Ni ngoma mpya na kali kutoka kwa Zuchu ambayo wiki hii imeshika nafasi ya nne. Ni ngoma kali ya mapenzi ambayo Zuchu amemshirikisha staa kutoka Nigeria, Adekunle Gold.
5. Amelowa
Ngoma ambayo pia ni kutoka kwa Harmonize imeendelea kuwa miongoni mwa ngoma pendwa kwa sasa kutokana na namna alivyoimba kwa kutumia lugha ya picha kwa kiasi kikubwa.
6. Cough (Odo) ft. Empire - Kizz Daniel
Baada ya kutamba muda mrefu na ngoma yake Buga (Lo Lo Lo), ngma nyingine ya Kizz Daniel 'Cough (Odo)' imeanza kutamba kwa kuingia kumi kumi bora ya 100 bora ndani ya app ya Boomplay.
7. Rush - Ayra Starr
Kwa mara ya kwanza, ngoma hii iliingia kumi bora wiki mbili zilizopita. Ni ngoma kali ambayo haichoshi kusikiliza. Endelea kusikiliza hapo chini.
8. Marry Me ft. Marioo - Barbana
Ni ngoma kutoka kwa Barnaba ambayo imeingia kwenye kumi bora ya chati za Boomplay takribani mwezi mmoja sasa. Ngoma hii ambayo amemshirikisha Marioo pia imetoka kwenye albamu yake 'Love Sounds Different'. Uwepo wa Marioo umeongeza utamu zaidi kwenye ngoma hii.
9. Mchumba - Nandy
Ni ngoma mpya kali kutoka kwa Nandy. Ngoma hii imependwa sana kutokana na midundo na miondoko yake. Hapa Nandy amekonga nyoyo za Watanzania wengi sana.
10. Leave Me Alone ft. Abigail Chams - Harmonize
'Leave Me Alone' kutoka kwa Harmonize ni bonge moja la ngoma. Hakika hapa Harmonize alituliza kichwa kweli kweli na uwepo mwanadada Abigail Chams ndiyo umezidisha mvuto wa ngoma hii kwa jinsi anavyoichezesha sauti yake.
Leave Me Alone ft. Abigail Chams
Wimbo gani umekuvutia kwenye orodha hii?
#BuzzBrandColumn #BoomTop #Music #Trending
Comments (16)
New Comments(16)
yohanafo1h5
Kulwa Masente9pvm4
good
GEOFTZ MNYAMWEZ1
kila ngoma imekaa kweny namba sahihi apo
phiaen0ar
kali
140603294
zotee kalii
Asquatic_iconic
✊✊
zainabu vicent
[0x1f633][0x1f633][0x1f633][0x1f633][0x1f633]
mato treems
hakuna ngoma fty hapa kama hakuna diamond platnumz and [0x1f602][0x1f602][0x1f602][0x1f602]
Yohana George komanya
daah zote fire
sabry _008
zote nzur
Drau Sanare
ngoma zote nzur
Yamsebo Kalangila
[0x1f633]
zuchu kwikwi imetixha mno