Mtoto wa Davido afariki dunia
Mtoto wa staa wa muziki nchini Nigeria, Davidi Adedeji Adeleke maarfu kama Davido Ifeanyi Adeleke mwenye umri wa miaka mitatu (3), amefariki Dunia Jumatatu hii baada ya kuzama kwenye Swimming Pool nyumbani kwao.
Vyanzo mbalimbali kutoka Nigeria vinaripoti kuwa Ifeanyi ambaye Davido amezaa na mpenzi wake Chioma Rowland maarufu Chef Chi, alizama kwenye Swimming Pool kwa muda mrefu kabla ya wazazi wake kugundua kutoweka kwa mtoto wao.
Baada ya kufanya msako mkubwa kuhakikisha wanampata mtoto huyo, walikuta Ifeanyi akielea kwenye maji.
Inaelezwa, juhudi za kumkimbiza hospitalini mtoto huyo hazikufanikiwa kuokoa maisha ya Ifeanyi ambaye tayari alikuwa ameshafariki.
#Trending #Davido
Comments (7)
New Comments(7)
Kelvin Mulokozi
Stevjohnson
R. I. P
Neema Chuwatz
rest in peace
MTALEMWA 1tnc
Pole
Lazaro mtisifbr5f
polen sana
mamushkacom37
So sad. RIP Ifeanyi
rehema Ebrown
mmh[0x1f653][0x1f653] soo sad[0x1f616]
R.i.p