New Music | Harmonize aachia albamu mpya 'Made For Us', ngoma gani kali zaidi?
Staa wa muziki nchini Tanzania na bosi wa lebo ya Konde Music Worldwide, Harmonize ameachia albamu yake mpya ambayo ameipa jina la 'Made For Us'.
'Made For Us' ni albamu ya tatu ya Harmonize tangu aanze kufanya muziki rasmi. Albamu hii inakuja takribani mwaka mmoja kupita baada ya albamu yake ya pili 'High School' ambayo aliiachia Novemba 5, 2021.
'Made For Us' ni albamu yenye jumla ya ngoma 14, huku baadhi ya ngoma hizo zikiwa tayari zilikwishaachiwa mapema kabisa kabla ya albamu hii kuachiwa. Ngoma hizo ni 'Amelowa', 'Nitaubeba', 'Deka', 'Miss Bantu', na 'Leave Me Alone'.
Ngoma zilizopo kwenye albamu hii ni 'Mwenyewe', 'My Way', 'Leave Me Alone', 'Wote', 'Nitaubeba', 'Utanikumbuka', 'I Miss You', 'Die', 'The Way You Are', 'Miss Bantu', 'Best Friend', 'Deka', 'Too Much' na 'Amelowa'.
Wasanii walioshitikishwa ni Abigail Chams, Bruce Melodies, Nak, Ntosh Gazi, and Spice, huku watayarishaji kadhaa mahiri wakishiriki kuhakikisha albamu hii inakuwa mahiri kabisa. Watayarishaji hao ni B Boy Beats, Dj Tarico, Daxo Chali, Paul Maker, Gachi, and Sign Beats.
Mpaka sasa albamu hii imefanikiwa kufikisha zaidi ya streams 250k kwenye app ya Boomplay. Sikiliza 'Made For Us' kutoka kwa Harmonize hapo chini kupitia Boomplay.
#Trending #Music #Harmonize #MadeForUs
Comments (11)
New Comments(11)
Costa mjapan
rizzojr88
zotee kalii apoh
dady7teen
all is gud music,,
shangegbmxd
my way best friend leave me alone nitaubeba deka and mwenyewe
sylvestermkama716@gmail.
[0x1f60e][0x1f60e] good job mr
mustapha salume8izd
ngoma zote atal
shija rajabu
kho kho
Emmanuel Charles07xm6
bestfriend
Yusla Elias
Aiseee zote kali[0x1f627][0x1f627][0x1f60e][0x1f60e]
BerryNipeys
Muzik
johnny francis
ngoma namba 4
hii ni qal ya zote biggest album ever