Boom Discoveries | Mfahamu Kontawa
Moja ya wasanii wa muziki wa rapa wanaochipukia kwa kasi kubwa nchini Tanzania, Kontawa ni miongoni mwao.
Kontawa ambaye mpaka sasa amefanikiwa kuachia ngoma 10 rasmi, amejaaliwa flow na vina vikali kwenye mistari yake, huku vikiambatana na ujumbe mzuri.
Kontawa ambaye kabla ya kuingia kwenye muziki alifanya shughuli mbalimbali ikiwemo kuuza mitumba, udalali na kadhalika amesema kuwa licha ya kuimba muziki wa rapa lakini bado ana uwezo wa kuandika mashairi ya muziki wa aina mbalimbali na kuongeza kuwa muziki ambao bado hajafanya mashairi yake ni Taarab na Reggae.
"Mimi napenda kusikiliza wasanii na muziki wa aina mbalimbali, sina msanii ambaye ndiyo pekee huwa namfuatilia kwa sababu napenda kupata vitu vipya kutoka kwa wasanii mbalimbali kila mara kwa ufupi sina itikadi kwenye muziki wangu." Kontawa ameiambia Boombuzz wakati akijibu swali la kwamba msanii gani ambaye amekuwa akimfuatilia zaidi.
Mbali na kupenda muziki, Kontawa amesema kuwa alikuwa na ndoto za kuwa injinia, hivyo hupendelea sana kufanya masuala ya mapambo na kuongeza kuwa huwa hajisikii vizuri anapokutana na mazingira ambayo sio nadhifu.
Kuhusu kusainiwa na lebo yoyote ikitokea wanamhitaji, Kontawa amesema kuwa ni suala la makubaliano na ikitokea makubaliano yana faida kwenye pande zote, basi hatakuwa na tatizo lolote.
Kwa sasa Kontawa anatamba na ngoma yake mpya inayojulikana kwa jina la 'Champion' na inapatokana kwenye app ya Boomplay, sikiliza hapo chini;
#BuzzBrandColumn #BoomDiscoveries #Music #Kontawa
Comments (1)
New Comments(1)
paloko66lyk
nice songs