MASTAA BONGO WALIOJALIWA WATOTO MWAKA HUU - 3
Tanzania
0
Vanessa Mdee
Mwishoni mwa Septemba Vanessa Mdee alijaliwa mtoto
wa kiume na kumpa jina la Seven, kabla ya hapo picha za
ujauzito wake zilichapishwa kwenye Jarida la People la
Marekani akiwa na Mchumba wake, Rotimi.
Wawili hao ambao walichumbiana mwishoni mwa 2020 wanaishi wote nchini humo mara baada ya Vee kutangaza kuacha muziki, taarifa za ujauzito wa Mwimbaji huyu zilikuwa za siri sana, hata tetesi zilipochukua nafasi aliibuka na kukanusha.
Malkia Karen
Baada ya kuwepo tetesi za muda mrefu kuwa ni mjamzito, mwishoni mwa Oktoba mwaka huu mwimbaji huyu alichapisha picha kwenye ukurasa wake Instagram zikimuonyesha akiwa mjamzito.
Hatua hiyo iliambatana na kuachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Haja, lakini hadi sasa hajaweka wazi kuhusu ni nani hasa baba wa mtoto wake huyo.
Mwisho, TU follow account YETU
#vanessamdee #MalkiaKaren #flsa
Comments (0)
0/500
New Comments(0)
What do you think of this post?