#BoomplayAwards: Aslay apokea tuzo tatu Boomplay
Nyota wa muziki nchini Tanzania, Aslay Isihaka 'Aslay' amefanikiwa kupata tuzo tatu kutoka Boomplay.
Aslay amepata tuzo hizo kupitia EP yake ya 'Kipenda Roho' ambayo imepata zaidi ya streams milioni 2, wimbo wa 'Likizo' wenye streams milioni 1 pamoja na streams za ngoma zake zote ambapo jumla yake ni milioni 10.
Mbali na ngoma hizo mbili kupata tuzo, Aslay pia amefanikiwa kupata tuzo ya kufikisha jumla ya zaidi ya streams milioni 10 kwenye ngoma zake zote kupitia Boomplay.
Haya ni mafanikio makubwa kwa Aslay kwenye mtandao wa Boomplay kwani ni moja ya wasanii ambao wamekuwa wakifanya vizuri kwenye app ya Boomplay.
Hii inatokana utunzi bora wa Aslay kwenye nyimbo zake nyingi, jambo linalowafanya wasikilizaji wa kila rika kuzikimbilia na kusikiliza mara nyingi kadri wanavyoweza.
Huu ni muendelezo wa Aslay kufanya vizuri Boomplay. Ikumbukwe mwaka jana, alifanikiwa kupata tuzo (plaques) nne. Ni dhahiri Aslay ataendelea kufanya vizuri na kupata tuzo nyingi zaidi kutoka Boomplay.
Kwa sasa, Aslay anatamba na ngoma yake mpya 'Fofofo' ambayo amemshirikisha msanii wa rap, Young Lunya. Unaweza kusikiliza hapo chini kupitia Boomplay.
Ngoma gani za Aslay ambazo ungependa kuona mwakani zikibeba tuzo?
#BoomplayAwards #Aslay #Music
Comments (44)
New Comments(44)
emmanuel ehuou
Odo Uko
OK o o o o o o o o o o o o o
JUMMAI ISAH
nice one
shijad9kg5
big up sanaaaaaa
sahim suleiman
seems like this gonna be to him
125950040
makin xana
mamushkacom37
Great
Salha Ally255
very goooood
Rom Peter Jr.
big up
godliven laizer
godliven laizer
ongera sanaaaaa[0x1f621][0x1f621][0x1f621][0x1f621][0x1f621][0x1f621][0x1f621][0x1f621]
Ommy Boyz
hongera sana kwa kaz nzur
get you boomplay reward points now