#BoomplayAwards: Rayvanny apata tuzo Boomplay!
Kwa sasa, Rayvanny ni miongoni mwa wasanii wakubwa nchini Tanzania. Hilo halina ubishi hata kidogo kutokana na staa huyo kutoka lebo ya WCB Wasafi kufanya vizuri kwenye kila jukwaa la kusikiliza na kupakua kazi za muziki.
Kupitia app ya Boomplay, Rayvanny ambaye ni mmiliki wa lebo ya Next Level Music amefanikiwa kujipatia tuzo (plaques) sita, jambo ambalo linaendelea kuthibitisha ukubwa wa muziki wake.
Tuzo hizo ni kupitia nyimbo zifuatazo; 'Tetema' ft. Diamond Platnumz, 'Naogopa', 'Ex Boyfriend', (kila moja imepata zaidi ya streams milioni 1), EP ya 'Flowers' imepata zaidi ya streams milioni 8, 'Number One' ft. Zuchu umepata streams zaidi ya milioni 5, huku pia akipata tuzo ya jumla kwa ngoma zake zote kufikisha zaidi ya streams milioni 20. Ikumbukwe kuwa, kwa sasa jumla ya ngoma zake zote zinakaribia streams milioni 50.
Kutokana na hilo, amejizolea mashabiki wengi ambao wamekuwa chachu kwake kuendelea kufanya juhudi za kusongesha gurudumu la muziki wa Tanzania na kuufikisha mbali zaidi.
Albamu yake ya 'Sound From Africa' imeendelea kufanya vizuri sana kwenye app ya Boomplay, ambapo mpaka sasa imefanikiwa kupata zaidi ya streams milioni 13.
Kwa sasa, Rayvanny anatamba na wimbo wake wa 'Sweet' ambao una zaidi ya streams 500k.
Kongole kwake Rayvanny. Sikiliza 'Sweet' hapo chini.
#Music #Rayvanny #BoomplayAwards
Comments (65)
New Comments(65)
Official Mp Barakadq3t4
Edwardem7zo
brother anajua so anakosaje kitu kam hicho...i
Keli Ther
cogs bro
Sar-jay
more wins
Doris Wanja
good
shazzy menzo
big up
Jackiline Benedictoeiwvm
nakukubari kaka vizuri
roddy_01
boomplay is the best of all[0x1f63f][0x1f63f]
holydes
united africa...divided we fall...lets push africa forward..keep it up
emmanuel ehuou
nice big up
Emmanuel Edwardekglk
hongela kaka
Edwin godfrey
madness
vvanny chui