SURRENDER Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2022
Lyrics
SURRENDER - AMBWENE MWASONGWE
...
Yesu, na "sarenda" mambo yangu kwako
Maana wewe u mwaminifu
Kweli naogopa kukabidhi haya
Nimekuja tuzungumze
Ulikuwa shujaa nilipokuwa vitani
Nilipoumwa njaa ulikuwa mkate
Nilipohitaji sadaka kwa fidia ya dhambi
Ulifanyika kondoo nikashinda kwa Nguvu
Uliwakemea waliponinyamazisha
Ukawazuia waliponidhibiti
Ukaonyesha njia katika ya hila
Ukategua fumbo nikashinda kwa Nguvu
~
Nakushauri mjue Sana Mungu wako
Ili uwe na Amani moyoni
Ndivyo hayo mema yatakujia
Ninaogopa usipofanya hivyo moyo
Utapoteza utulivu wa ndani
Utahangaika na kuumia
Utapata taabu Sana wee moyo
Ukiwa bize kuchunguza watu na vitu
:::::::::::-:::::::::::::
Nimefanya kosa kuhesabu vya mwilini
Na kujidhania maskini
Kumbe nina utajiri wa rohoni
Unaozidi vya mwilini
Wewe umenipa vitu pesa haiwezi nunua
Umegawa bure vya thamani visivyo na bei
Pumzi, usingizi, hamu ya kula
Na afya
Kitanda, chakula na dawa visingeweza kunipa
Nitanunua bunduki
Sitanunua uhai
Nitanunua zawadi
Ila sio kupendwa
Nitanunua dawa
Ila sio uzima
Nitanunua mapambo
Ila sio uzuri
::::::::-:::::::::
Sitayaogopa yatishayo wanadamu
Wayaonayo ni makubwa
Ninakuamini Mungu wangu
Uwezaye kumeza kimezacho tembo
Wewe huyawazi yale yanipayo mawazo
Unawaza mema yaletayo Amani, Tumaini
Katikati ya magumu kana kwamba napoteza
Hata katika hayo nauona Wema wako
Wewe hutangazi yale sisi Twatangaza Sana
Twatangaza jambo mwanzo pale likishatokea
Wewe unatangaza mwisho wa jambo tangu mwanzo
Nitaficha ujinga wangu
Kukumbuka kukaa kimya
~
Nakushauri(moyo) mjue Sana Mungu(sikiliza) wako
Ili uwe na Amani moyoni (kama unatakaka)
Ndivyo hayo mema yatakujia (utulivu)
Ninaogopa(moyo) usipofanya hivyo
Moyo utapoteza utulivu wa ndani
Utahangaika na kuumia
Utapata taabu Sana wee moyo
Ukiwa bize kuchunguza watu na vitu
Nakushauri mjue Sana Mungu wako
Ili uwe na Amani moyoni
Ndivyo hayo mema yatakujia
Ninaogopa usipofanya hivyo
Moyo utapoteza utulivu wa ndani
Utahangaika na kuumia
Utapata taabu Sana wee moyo
Ukiwa bize kuchunguza watu na vitu
:::
Utapata taabu Sana wee moyo
Ukiwa bize
Kuchunguza
Watu na vitu
*