Mbosso aanika siku ya uzinduzi wa EP yake mpya
Staa wa muziki kutoka WCB Wasafi, Mbosso ametangaza rasmi kufanya uzinduzi wa EP yake mpya Alhamisi hii, Oktoba 27, 2022.
Mbosso ametanabaisha hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo amesema atafanya uzinduzi huo katika fukwe za Barra Beach, Dar es salaam.
"Alhamis Hii October 27 nitakuwa na Launch rasmi Ep Yangu katika fukwe za @barrabeachtz “ Bahari Beach” Dar Es Salaam kuanzia Saa 12 jioni nikiambatana na Rafiki Mbalimbali , Kaa na Mimi kujua Unapataje Mualiko wako…ila je, we Unadhani Ep itakua na Nyimbo Ngapi na inaitwaje?" Mbosso ameandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.
Kwa mujibu wa Mbosso, hii ndiyo project yake atakayofungia mwaka huu wa 2022 lakini hajabainisha jina wala idadi ya nyimbo zitazokuwa ndani ya EP hiyo.
Nini mtazamo wako?
#Mbosso #Trending #Music
Comments (2)
New Comments(2)
GSU CEO and Company Limited
ZiO Drop®
fundii[0x1f63f][0x1f63f]
anajua huyoo dogoo