Killy na Cheed waondoshwa Konde Gang
Uongozi wa Konde Music Worldwide maarufu kama Konde Gang umetangaza rasmi kusitisha mikataba na wanamuziki waliokuwa chini ya lebo hiyo, Cheed pamoja na Killy kutokana na sababu mbalimbali zilizo nje ya uwezo wao.
Lebo hiyo ambayo leo imetimiza miaka 4 tangu kuanzishwa kwake Oktoba 10, mwaka 2019, iliwasainisha Cheed na Killy Septemba 2020 wakitokea lebo ya King’s Music ya mwanamuziki Alikiba.
Wasanii hao wamedumu kwa kipindi cha miaka miwili tangu kusainiwa chini ya lebo hiyo.
Wakiwa Konde Gang, Cheed na Killy kila mmoja amefanikiwa kutoa EP yake na kumshirikisha Harmonize. Cheed aliachia 'Endless Love', huku Killy akiachia 'The Green Light'.
Nini utakumbuka kutoka kwa wasanii hawa wakati wakiwa Konde Music?
#Trending
Comments (16)
New Comments(16)
jimmy kajoller
Loveness Godlove
ndio kwanza nawasikia leo sinawahi hata kiwasikia
Angel xz2l5
Mung awajaaliee
beate22
tunawatakia safari njema
King tony 09i1o
Ilikuwa sio sehem sahihi kwao mana promotion ya mziki wao it was very inadequate to them [0x1f637]
rayyanpzfnr
mungu awasaidie
@issa_og
laana za kiba znawatafna[0x1f604]
chefcooker
afadhali maan future yap ya mziki ingekufa zaidi wakiwa pale,,hawapewi time na promotion kama anavyojipa harmonize mwenyew,ye kila week nyimbo alaf wasanii wake hata miezi sita hakuna kazi na hata wakitoa kazi bado ana wa ingilia kati na .yeye anatoa ngoma kabla ngoma za wasanii hazijafika mjini
Jesca Robert8ea49
Acha waende mana mm nilikua sion umuhim wa likua tu wanatujazia choo kwa konde wetu
Ngassa Edward
acha nao
femaleflkvx
CHIBA 47
femaleflkvx
waludishwe konde gang wana vipaji
konde gang waache uwongo basi inaama ata awo jamaa wakipatwa na misiba pia awata husika ama ndio mikataba yakiswahili ikiisha na undugu unaishaa